Sunday, November 15, 2009

HUDUMA ZA AFYA ZIBORESHWE HASA KATIKA VITUO HIVI

Tunapozungumzia huduma za jamii tunazungumzia mashule, hospitali barabara na vyombo vya usalama

Na ukiweza kuvitimiza hivyo kwa wakati wake ndio mwanzo wa maendeleo na kama kimoja kitayumba ni wazi kuwa hakuta kuwa na maendeleo

Kwa Tanznia serikali inajitahidi kuwafikishia wananchi huduma hizi kwa ukaribu sana ili kuwasogezea maendeleo karibu zaidi

Lakini hivi itakuwa na maana gani kama kutawa na majengo lakini pasiwepo na vifaa vinanyotarajiwa kuwepo ? mfano shule ili iwe shule ni lazima iwe na vifaa vya kufundishaia pamoja na walimu wa kutosha

Na kwa upande wa hospitali kuwe na mahabara vipimo vya kutoosha na madawa ya kutosha tofauti na hayo hiyo basi sio huduma

Ipo hospitali moja ya serika iliopo Tabata Segerea ambayo kimsingi ni nzuri na ni mpya kwa maana ndio imefunguliwa lakini pia tunaamini kuwa labda hata wafanyakazi wake ni wazuri .

hii inatoka na ukweli kuwa kitu kipya hata mambo yake ni mapya hivyo watu kukimbilia wakijua watapata yalio bora

Lakini swala la kushangaza hata kama una kila dalili ya ya maleria ambayo kila mtu wa kawaida anaweza kuiona lakini wakikupima wanakuambaia eti huna maleria

Lakini ukipima maleria hiyo katika vituo vingine vya afya utakutwa na wadudu kibao wa maleria

Swala hili limekuwa la kawaida sana katika hospitali ile ambapo kama hawatajali hawatakuwa na wadau lakini pia wanaweza kuhusika na matatizo endapo yatatokea

Lakini kwa ukweli hivi vipimo havisomi ukweli au vipimo vimeharibika au hakuana watu wenye uwezo wa kutumia mashine hizo hivyo wanashindwa kuvisoma ?

Maswali mengi kamahaya yamekuwa yakiulizwa na weatua wengi sana na si zani yupo ambaye emepata majibu

Tuesday, November 3, 2009

HI NI KWELI MAENDELEO NI LAZIMA YAVUNJE MAENDELEO?

Katika kipindi hiki kumekuwa na matatizo ya miundombinu ya bara barahasa za mitaani kutokana na utengenezaji wa miundombinu ya mabomba

Wachina wamekuwa wakijaribu kutengeneza miundombinu ya maji hapa DSM ambayo kila barabara imeharibika katika mitaaa na kutokana na jinsi wanavyochimba mitaro na kuiacha bila ya kuifukia

Ukiangalia katika mtaa ya tabata segerea kimanga na penginepo watu huwa hulazimika kulaza magari yao CCM na wengine na kuharibika kwa magari yao

Sasa nawajiuliza kwanini barabara ifungwe kwa tatizo lijalo, kwa nini ukichimba usifukie?
kwa ni lazima maendeleo ya vunje maendeo mengine?
kwa ni lazima miundombinu mipya ivuruge miundo mbinu ya zamani?

Tujirekebisheni

Matatizo ya waislam hayakuanza leo wala njana

Katika historia uislam uliletwa hasa huku afrika na kuenezwa na waarabu

Pia iliaminika kuwa ulikuwa na nguvu sana kuliko dini nyingine lakini kwa ukweli ni kwamba waarabu walikuwa wafanya biashara wazuri na walikuja na elimu lakini ilikuwa na ni elimu ya dini tu

Baadae ndipo walipokuja wamisionari na dini yao ambayo ndio dini ya kristo

Ujio huu wa wamisionari ulikuja na dini, utawala na elimu ya zaidi

Swala ambalo lilifanikisha kuwamiliki waarabu walikuwa wakisambaza dini ya kiislamu

Hii ilitokana na ukweli kwamba wamisionari hao ndio waliokuwa watawala hivyo kuwa na nguvu sana na kuweza kuzima baadhi ya dola za kisilim

Kutoikea enzi za ukoloni ukristo popote duniani umekuwa ukipata misaada ya kifedha na kimawazo kutoka katika mataifa mbalimbali ili kuimarisha utawala wao

Kwa kuwa kipindi chote hicho wakristo walikuwa ndio watawala hata misingi ya elimu waliishikilia wao hivyo ndio waliokuwa na dhamana ya nani apate elimu na nani asipate

Hivyo utaratibu ulikuwa kwamba usiekuwa mkiristo ukitaka elimu basi uwe mkristo mbali na hivyo elimu hupati

Mbinu hii iliwarudisha sana walikuwa tofauti na wakrito na himaya za wakristo zilipata nguvu sana hadi leo

Katika kuimarisha dini ya wamisionari walitumia sana propaganda katika kupata wadau wengi kutokana na nguvu ya neno propaganda yenyewe ilivyo

Propaganda hizi zilitumika katika kuwatia watu woga hasa katika dini ya upande wa pili na kwa wengi walio amini waliaanza kuona uislam kama dini ya shetani,dini ya watu wasiokuwa na elimu na hata kuiona kuwa dini ya kigaidi

Hali hii imeendelea hadi leo ndio maana utakuta waislam kila wanachotaka kukipata kina kuwa kwao ni shida tupu

Mataifa makubwa yanautambua uislam kuwa ukipewa nguvu basi huenda wakakumbuka shida waliopata hivyo hivyo wakalipiza

Haya hanaasababisha Taasisi nyingi sana za kiislam kuvunjika au kutoendela kwani misaada yote ikitolewa na waislam inaitwa ya kigaidi

Waislam wallitaka kujiunga na NIC ilikuwa shida makinisa yakisimamia kidete sasa waislam wanataka kuanzisha mahakama ya kadhi ambayo ki msingi hii ni kwa ajili ya waislam ili kutafuta haki zao za kiislam lakini hata wasiokuwa waislam wana kataa kwa nguvu mi nafkiri kuwa hapa kuna tatizo

Hivi wewe ungepata nafasi ya kutoa amoni yako kuhusu hili ungesemaje?

Monday, November 2, 2009

UCHAGUZI WA MWAKA 2010 NA KIWANGO CHA ELIMU

Uchaguzi wa 2010 na elimu

Katika uchaguzi wa mwaka 2010 utakuwa wa kipekee kuliko chaguzi zote ambazo zimetokea hapa Tanzania kutokana na kulenga wanajua kusoma na kuandika tu.

Kwa dondoo za uchaguzi ujao kwa wale wasiojua kusoma na kuandika hawatapata nafasi ya kuwachagua viongozi wao kwa kuwa fomu za kupigia kura zinamtaka kila mpaga kura kuandika majina ya wagombea wake tofauti na vipindi vilivyopita ambapo watu walikuwa wanaweka alama ya tiki

Hayo yamebainika jana baada ya wagombea wa nafasi ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kata ya Segerea mtaa wa Ugombolwa bibi Mariam Machicha kwa tiketi ya cha cha Mapinduzi CCM alipokuwa anaongea na wanachama wakati wa kampeni za chama chake

Alisema utaratibu huu wa kuandika majina ya wagombea katika kupiga kura umetoka ofisi ya Waziri mkuu TAMISEMI kwa makubaliano ya vyama vyote vya siasa hivyo hauwezi kubadilika kwa urahisi

Ni wazi kuwa utaratibu huu unawatenga watanzania wasiojua kusoma na kuandika kupata nafasi ya kutumia haki yao ya msingi ya kumchagua wamtakaye

Hata hivyo inaonekana kuwa elimu imechukua nafasi yake kwani kutokana na jamiii kuwa imeelimika kwa kiasi kikubwa inawapasa wagombea wenyewe wawe ni wenye elimu ili kukabiliana na changamoto zilizopo

MAEMBE NI UTAJIRI MKUBWA

Na Bashir Salum
Waswahili husema eti rizizki ya Mbwa ipo miguuni mwake,usemi huu unamaana kuwa riziki ya mtu ipo katika nafasi aliyo nayo na uwezo alionao

Maembe yaliopo Tanzania yanaweza kubadilisha na kumuongezea riziki ya mkulima wa Tanzania kama akielimishwa vizuri kuhusu ukulima bora na wa kisasa

Maembe yanaweza kumnyanyua mkulima kwa kumuongezea kipato na kuboresha maisha ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi wa nchi.

Utayarishaji wa shamba la miembe,mkulima anashauriwa kuandaa shamba mapema, kutumia mbegu na miche bora iliyofanyiwa utafiti na vituo vya utafiti hapa nchini.

Mikoa yote inalima miembe ila inatofautiana kwa kiwango cha uzalishaji kutokana na tofauti za maeneo hayo

Zao hili linalimwa katika mikoa yote kwa sababu ya uwezo wake wa kustawi katika aina mbalimbali za udongo na kustahimili aina mbalimbali za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na ukame.

Miembe inaweza kustawishwa mahali ambapo aina nyingine nyingi za mazao haziwezi kustawi.

Zanzibar ilishazalisha jumla ya Tani 6,546. Kiasi hicho cha embe kilivunwa katika mashamba yenye jumla ya eneo la Hekta 1,372

Ingawa miembe imepandwa Zanzibar katika eneo lenye jumla ya Hekta 1,734 na kaya zilizohusika na kilimo hiki ni 12,819.

Ingawa takwimu hizo hazikuonesha kuwa sasa Tanzani iko nafasi ya ngapi katika uzalishaji wa zao la embe ,

Hata hivyo zinaonesha kuwa kuna ongezako la Tani 146,028 katika kipindi hicho. Ambapo maembe mengi yamezalishwa hapa Tanzinia

Soko la maembe limekuwa kwa kiasi kikubwa duniani ikiwa ni moja ya sababu ya kuongezeka wataalamu wa maembe

Kuna aina zaidi ya 140 za embe ambazo hupatikana hapa tanzania na duniani kwa ujumla kulingana na mazingira yake
.
Ubora wa embe unatofautiana kutokana na sifa za embe na aina ya embe husika ijapokuwa kila embe lina ubora wake.

Sifa hizo zipo nyingi sana, hata hivyo ili kurahisisha kuzitofautisha baadhi ya embe zinazojulikana zaidi katika masoko Tommy Atikns KEITT na kent zill aina hizi ni nzuri sana

Hukomaa mwanzoni hadi katikati ya msimu Matunda yake ni makubwa, huweza kufikia kati ya gramu 450 hadi 700 Umbile la tunda ni kati ya umbile la yai na mviringo
Likikomaa huweza kukaa muda mrefu bila kuharibika Tunda lina rangi nyekundu ambayo haijakolea na imechanganyika na njano na Lina utamu wa kadiri

Zipo aina nyingi za maembe zilimwazo na wakulima hapa nchini kama vile embe dodo, bolibo, sindano, zafarani, mviringa na nyingine nyingi ambazo tumezizoea.

Aina hizo za maembe uzalishaji wake ni mdogo lakini wataalamu wameweza kuingilia kati tatizo la uzalishaji mdogo kwa kutumia mbinu ya ubebeshaji wa maembe.

Ubebeshaji wa maembe ni njia sahihi katika kuhamisha sifa halisi cha maembe kutoka kwenye mche unaotoa mavuno mengi bila kuathiri sifa na tabia za embe unalokusudia kupata.

Mbinu hiyo hutumia shina mama lenye sifa ya kutafuta chakula kwa wingi ardhini na hubebeshwa na aina nyingine inayokidhi mahitaji ya mkulima kwa kumpa bei nzuri.

Matokeo ya utumiaji wa mbinu hiyo ya ubebeshaji wa maembe sasa kuna aina mpya za maembe zinazoweza kupenya soko la maembe la kimataifa.

Aina hizo ni Red, Apple, Alphoncal ambazo tayari zimepiga hodi kwa wakulima wa maembe wa wilaya ya Mkuranga.

Mbali na hayo kuna aina ya miembe inayokidhi sifa hizo ni pamoja na Kent, Keith, Tommy Atkins, Alphonso, Sabre, Van Dyke, Apple, Ngowe na Red Indian (Zill).

Wakulima walio karibu na bustani zinazomilikiwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika pamoja na zile zilizoko chini ya manispaa wameanza kupanda aina mpya za maembe.

Bustani zinazomilikiwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kupitia kitengo chake cha promotion ya mazao zipo Mpiji wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani,

Bustani ya Manispaa Ilala yenye aina mpya za maembe ni ile ya Kinyamwezi ambayo ipo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kupitia Gongola Mboto kuelekea njia ya Chanika,Pia zipo nyengine ambazo zipo maeneo ya Lushoto na Muheza Tanga

Wakulima wengi hawajui kanuni bora za kilimo cha maembe na hivyo kuwafanya wakulima kutoyaona manufaa ya maembe

Tatizo kubwa linalo kabili uendelezaji wa zao la embe ni kutopatikana kwa miche ya kutosha ya miembe bora.
Pia bei kubwa ya miche ambayo, huuzwa kati ya shilingi 2,000/= na 3,000/= kwa mche

Ili kuondoa tatizo la upatikanaji wa miche bora ya miembe Wizara ya kilimo chakula na ushirika imeweka mkakati wa kuongeza uzalishaji wa miche hiyo na upatikanaji kwa wakulima.

Miche hiyo bora ina sifa za kuzaa maembe mengi kwa eneo na yenye ubora unaokubalika katika masoko yetu ya humu nchini na yale ya nje ya nchi.

Wapo wakulima ambao wanawezeshwa kuanzisha mashamba ya miembe bora kwa kupewa miche bora ya miembe na kupanda katika mashamba yao.

Miembe imepandwa katika mikoa ya Pwani, Morogoro na Dodoma na sehemu nyingine hapa nchini.

Mashamba hayo yanakuwa ni mashamba ya mfano ambapo wakulima wanayatayarisha mashamba kwa kufuata kanuni zote za kilimo bora cha miembe.

Mashamba hayo yatakuwa ni sehemu ya kuwafundishia wakulima wengine kwa kuona aina mbalimbali za miembe bora jinsi inavyoweza kuzaa maembe yenye ubora zaidi

Baada ya miaka mitatu miche hiyo itaanza kuwa tayari kutoa vikonyo ambavyo vitatumika kuzalisha miche mingine unaofanywa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika katika kuendeleza zao la embe.


Jumla ya miembe bora 5,141 imezalishwa na kupandwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili kuwafaidisha wakulima

Miche 595 ya miembe bora imepandwa Dodoma Vijijini huko Chamwino katika Tarafa ya Mvumi na vijiji vake, Makulu miche 200, Ilolo miche 100, Muungano miche 100 na miche 195 ilipandwa Ikowa Dodoma.

Pia Miche 150 imepandwa katika Kituo Cha Amani kijiji cha Makang’wa Dodoma,Miche 120 na kijiji cha mwambaya wilayani Mkuranga

Pia wapo wkulima ambao watagaiwa Miche mingine 400 wilayani Mkuranga namiche 250 itakayo gaiwa Morogoro.

Hata hivyo jumla ya Miche 3,500 ya miembe bora imezalishwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushika kwa kushirikiana na wanachama wa Chama cha Wakulima wa Miembe ili kuwanufaisha wakulima

Miche hii ya kisasa inachukua miaka miwili na nusu kuanzia kupanda hadi kuzaa ile ya zamani inayochukua miaka mitano had saba kupanda hadi kuzaa

Kila mwaka idadi hiyo ya miche itakayozalishwa itakuwa inaongezeka kwa zaidi ya mara mbili Mashamba hayo ni ya wakulima wenyewe ambapo yanakuwa na malengo makuu matatu yafuatayo


Kama wakulima watatilia mkazo kwenye zao hili kwa kutumia mbegu sahihi za maembe zinazo zaa sana na kuchukua mda mfupi wanaweza kuondokana na umasikini

Mkoa wa pwani hivi karibuni uliweza kujionea mradi wa maembe ulikuwa umetembelewa na Raisi Jakaya Kikwete unaomilikiwa na Dkt. Salum Diwani

Shamba lililokuwa limesheheni miembe mingi ya kisasa iliyokuwa imezaa vizuri ilikuwa ni changamoto kwa yeyote alikuwepo kwenye mkutano huo kulima maembe

Iliwekwa wazi kuwa soko la maembe hayo linapatikana nchini Tanzania na nchi za jirani kulinga na ubora wake

Raisi Jakaya Kiwete alitoa changamoto kwa wizara ya kilimo chakula na ushirika kuandaa program maalum kuendeleza kilimo cha maembe katika mikoa inapostawi

Ilikadiriwa kuwa mti mmoja mkubwa wa mwembe huweza kutoa maembe hadi 3000 na midogo hutoa maembe 300

Huu ni utajiri kwani mkulima akilima miti kumi ikazaa vizuri midogo inaweza kuzaa maembe elfu tatu 3000 na mikubwa kutoa maembe elif thelathin 30,000

Hivyo mkulima akiuza embe moja kwa shilingi 300 huweza kupata kati ya 900’000 na 9,000,000 kwa miembe mikubwa na midogo

Mkulima angeweza kufaidika sana na kilimo cha maembe na hata kuitambulisha nchi kimataifa

Kuna mradi ujulikanao kama common Fund for Commodity ambao Tanzania na Zimbabwe ni wanachama na wamepewa furusa ya kuandaa mazao ya biashara ya kuuza nchi za nje

Soko la miembe hapa Tanzania lipo isipokuwa wanunuzi kutoka nje wanahofia kufanya biashara na watanzania kwa kile wasemacho kuwa hawjajipanga kutojitosheleza
Wenyewe

Yupo Inzi ajulikanaye kama inzi maembe kwa jina la kitaalamu bactrocera invadens husababisha funza ambao huharibu maembe

Funza anayejitokeza baada ya mayai kuanguliwa huishi kwa kula nyama ya maembe na kusababisha vidonda ndani ya embe na matokeo yake ni kuoza kwa embe.

Mara nyingi funza huchangia kwa kiasi kikubwa kushusha thamani ya embe na kufanya soko lake kuanguka

Wadudu wanachangia kuharibu soko la embe kutokana na kufanya embe kuoza mapema kabla ya kuiva na kupelekwa sokoni

Wapo wadudu mbalimbali ambao wanaweza kuharibu maembe kama vile Inzi ambao hutoboa na kutaga mayai ndani ya embe na husababisha embe kudondoka mtini

Tuna wakulima wengi wa maembe sehemu nyingi hapa Tanzania kama Kilimanjaro Tanga na hata Morogoro ambapo mda sio mrefu watakuwa na elimu kuhusu kilimo cha maembe

Ijapokuwa sio wakulima wote wana elimu kuhusu kilimo endelevu cha maembe na magonjwa yanayo athiri zao la maembe lakini elimu hawezi kuwa kuta wote kwa wakati mmoja

Watalaam wa Wizara pamoja na wa Halmashauri huvitembelea vijiji mbalimbali na kukutana na serikali ya kila kijiji husika ili kuwaewesha kazi inayokusudiwa kufanyika katika vijiji vyao.

Katika hatua zote ushirikishwaji wa wakulima unazingatiwa ili kukifanya kilimo hiki kuwa endelevu.Ili kutimiza azma hiyo Wizara imekwisha fanya mabo mengi mfano

Wizara imekiimarisha Bustani ya kuzalisha miti ya matunda ya Mpiji huko Bagamoyo pamoja Pampu za maji 5 ambazo zimenunuliwa.

Matenki ya maji 5, moja la lita 3,000 na manne ya lita 2,000 kila moja yamenunuliwa ili kukizi mahitaji muhimu.

Watanzani tuna takiwa kuiga mfano wa Colombia ambayo huwa inapata dola za marekani mill.200 kwa mwaka kwa kuuza maembe Ulaya pesa ambayo kwa Tanzania ni sawa na mazao mawili

Ili kufikia lengo la kukuza soko la maembe kwa, mkulima anatakiwa kupalilia shamba lake pamoja na kusambaza dawa za mda mfupi

mwisho

rasilimali za mkoa wa kilimanjaroa lakini...

Na Bashiri Salum
Watu husema umaskini ni sawa na mzigo wa mzoga ambao kama hutautua kwa ajili ya harufu yake basi utautua kwa uzito wake.

Haya ndio yanayowakuta watu wa Kilimanjaro ambao wana rasilimali ambazo hawazitumii.

Mkoa wa Kilimanjaro unatakiwa kutumia mbinu za ziada ili kuutua mzigo wa upungufu wa chakula unaoikabili mara kwa mara.

Upungufu wa chakula unao ukumba mkoa wa Kilimanjaro unaweza kuzuiliwa kwa kuboresha kilimo, ufugaji na kuanzisha vyama vya akiba na mikopo.

Kutokana na kutegemea mvua za msimu wakulima mkoani Kilimanjaro wamekuwa wakishindwa kupata mavuno ya kutosha kutokana na uhaba wa mvua.

Wakulima wadogowadogo inafaa wawe wanatafuta pembejeo za kilimo kulingana misimu waliyonayo mkoani Kilimanjaro.

Naibu waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh Christopher Chiza alisema kuwa
kilimo cha umwagiliaji ni moja ya mikakati itakoayowezesha mkoa wa Kilimanjaro kuepukana na njaa

Mkurugenzi wa Idara ya usalama wa chakula , Bi Sophia Kaduma wakati wa mdahalo wa kampeni dhidi ya njaa alisema kuwa mikakati shirikishi inaandaliwa ili kusaidia mikoa hiyo hasa Mikoa ya Kilimanjaro na Singida ilyokumbwa na ukame


Mbali ya ushirikishwaji wa wananchi katika kilimo cha umwagiliaji serikali pia itahakikisha kuwa pembejeo za kilimo, dawa na ruzuku kwa wakulima vinawafikia kwa muda unaotakiwa

Mbegu za mda mfupi na zenye kutoa mazao mengi pia mazao yanayovumilia ukame kama mihogo na mtama yapewe kipau mbele kwa wakulima wa mkoa wa Kilimanjaro ili yaweze kuondoa upungufu wa chakula

Wakulima wengi mkoani hapo hutegemea kilimo cha mvua na wachache sana kutegemea kilimo cha umwagiliaji ambacho hupatikana zaidi katika sehumu za tambarare kwa msaada wa maji yatokayo kwenye misitu mbalimbali kama vile shengena, kindoroko na mlima kamwala na ile yam lima Kilimanjaro

Pia ardhi ya sehemu kubwa ya mkoa huo imechoka sana kutokana na kulimwa kwa mda mrefu bila ya mbolea na hata kuongezeka kwa idadi ya wakazi


Wakati nikiwa Mkoani Kilimanjaro katika wilaya ya Mwanga nilikutana na mzee mmoja aitwae Sawaya Mchwangondo Marisa (85) wa Usangi Vuagha aliweza kunieleza yafuatayo

Historia inaonesha kuwa Mkoa wa Kilimanjaro kila mwaka unaoshia na 4 au kugawanyika kwa nne lazima kuwepo na ukame pamoia na njaa ambayo huathiri sana uchumi wa Mkoa wa Kilimanjaro

Mwaka 1964 Mkoa wa Kilimanjaro ulikumbwa na njaa ambayo wakazi wa mkoa huo hususni wapare waliita njaa ya mkebe kutokana na vyakula vya msaada kupimwa na chombo kiitwacho mkebe

Mnamo mwaka 1968 ilitokea njaa lakini ilikuwa sio njaa kubwa kuliko ile iliotokeo mwaka 1974 ambayo chakula kilichokuwa kinapatikana ni mihongo na yenyewe ilikuwa inapatikana kwa uchache zaidi

Lakini hata hivyo kuanzia mwaka 1978 hali ya chakula ilikuwa sio nzuri ijapokuwa watu wachache wategemeao kilimo peke yake waliathirika zaidi kutokana na mavuno kupatikana lakini yalikuwa kidogo yasiokidhi haja za wakulima

Mwaka 1984 imeelezwa wazi kuwa upungufu wa chakula ulitokea Mkoani Kilimanjaro ulikuwa ni wa kutisha katika kipindi chote ambacho njaa ilshawahi kutokea

Serikali ya mwalim Juliasi Nyerere ulichukua hatua za kuaagiza chakula kutoka nje kilichojulikana kama mahindi ya Yanga(njano) Kwa kipindi hiki Taifa zima lilikuwa na hali mbaya sana ya chakula

Imekuwa kawaida watu wa mkoa huo kuamini kama kila mwaka utakao kuwa unnaishia na nne au nane kwao itakuwa na uhaba wa chakula hivyo mwaka 2008 inafahamika kuwa kutakuwa na upungufu wa chakula

Upungufu wa chakula mkoani Kilimanjaro huwa unasababishwa zaidi na ukosefu wa mvua za uhakika katika kipindi kizima cha mwaka na ukosefu wa elimu ya kuhifadhi chakula


Hata kiwango cha maendeleo kilichofikiwa na Mkoa wa Kilimanjaro kama ujenzi wa nyumba mashule, hoteli na miundo mbinu huwa ni moja ya mambo yanayochangia uharibifu wa mazingira yanayochangia kuchoka kwa aridhi

Kutegemea kilimo cha mkono kwa wananchi wengi mkoani Kilimanjaro ni moja ya sababu zinazofanya kutokea kwa upungufu wa chakula ambao hurudisha nyuma kasi ya maendeleo mkoani hapo.

Wakulima wengi wamekuwa hawatumii mbegu sahihi ambazo hazijahakikiwa na wataalamu kwa ubora hivyo kufanya mkulima kutopata mazao ambayo yangemtosheleza katika maisha yake

Pia sehemu nyingi za mkoa wa Kilimanjaro hawana elimu juu ya programme ya maendeleo ya sekta kilimo yaani ASDP ambayo ingeweza kuwasaidia wakulima wengi na kuwawezesha kuondokana na njaa.

Wananchi wa mkoa huo wanatakiwa kutumia mfuko huo wa ASDP katika kuibua miradi mbalimbali ili aweze kupanua uwigo wa upatikanaji wa chakuala na kufanya maisha kuwa marahisi

Mfano katika vijiji vya kata ya Jipendea ambapo hupata maji kutoka sehemu za milimani ikiwemo Usangi, Ugweno na Kilomeni wangeweza kutumia ile asilimia 75 ya uwekezaji inayotolewa na serikali na wahisani kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji

Upo muhimu wa kuongeza idadi ya mabwanashamba ili kuhakikisha kuwa kilimo kinaendelezwa kiufanisi ili kuepukana na majanga ya njaa

Ijapokuwa kunawafugaji ni wengi mkoani Kilimanjaro lakini wanategemea kilimo zaidi ya ufugaji

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bwana Abrahamani Babu alisema kuwa wafugaji wa mkoa huo wauze baadhi ya mifugo yao ili waweze kununu chakula cha kutosheleza mahitaji yao

Yupo mtaalamu wa mifugo aitwae DR BSJ Msangi wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo alisema kuwa changamoto zinazowakumba wafugaji wa Mkoa huo ndizo ambazo kumnyima mfugaji na mkulima kufaidi matunda ya kazi yake na kushindwa kujikomboa na njaa za mara kwa mara

Hata ivyo alisema kuwa upande wa soko la nyama sio taizo ijapokuwa lipo moja la Mgagau ambalo linategemewa na wafugaji wengi wa vijijini na mjini.

Hivyo soko la mifugo ndani ya Mkoa huo sio zuri la kumuwezesha mkulima au mfugaji kuweza kutegemea mifugo ili kuondoa uhaba wa chakula unao wakumba mara kwa mara

Serikali inampango wa kuanzisha namna ya usindikaji wa maziwa ili mfugaji kuweza kupata manufaa kupitia kwenye maziwa na

Lakini ikumbukwe kuwa kuuza mifugo sio suluhisho la kuondoa njaa, kutokana na kuwa gunia moja la mahindi ni kata ya shilingi 280000 na 30000 na bei ya ngombe mmoja ni kati ya laki moja na nusa (150000) na laki mbili (200000) ambapo ni sawa na magunia 5 na magunia 6

Kiasi hicho hakiwezi kuhudumia mahitaji ya familia kama chakula, mavazi,ada ya shule na kujitibu upatapo magonjwa kwa muda wa mwaka mzima


Mifugo inayopatikana mkoa wa Kilimanjaro haiwezi kuondoa njaa kutokana uhaba, na udhaifu wa mifugo yenyewe

Ukame unapo tokea sehemu husababisha Mazao ya chakula kuwa na bei ya juu, mazao mengine ka mifugo yanashuka bei kutokana na ukosefu wa pesa na malisho kwa mifugo

Kwani ukame husababisha mifugo kufa au kukosa afya hivyo kuuzwa kwa bei ya chini ili kukwepa kuwapoteza kabisa

Hivyo ukame unapotokea sehemu Fulani ,mifugo haiwezi kuondoa njaa kwa sababu hata yenyewe huwa inaathirika na ukame na hivyo soko lake linapungua

Hata hivyo wafugaji wengi wa mkoa wa Kilimanjaro hawajawezeshwa kufuga il kupata manufaa ya mifugo yao lakini wao hufuga kama sehemu ya utamaduni wao

Mifugo yao mingi haipatiwi chanjo za magonjwa na hawana elimu ya ufugaji wa kitaalamu ambao ungewawezesha kupata manufaa ya ufugaji

Ili wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro uondokane na njaa za mara kwa mara mbali ya kushiriki kilimo cha umwagiliaji wanatakiwa kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa ili kupata mitaji na kuboresha mifugo yao ikiwa ni pamoja nakupata chanjo za mifugo yao

Mkoa wa Kilimanjaro ni mojawapo ya Mikoa ambayo ina wasomi wengi kuliko Mikoa mingine wataalamu hawa wanatakiwa kushirikiana na kuwashauri na kutoa utaalamu wao ili kuondoa tatizo hili ambalo limekuwa likijirudia kila mara

Katika Tarafa ya Usangi Mkoani Kilimanjaro msimu wa maharage huvunwa kwa kiasi kikubwa lakini wakulima huyauza, tena kwa gharama ndogo, hivyo Serikali za Mitaa zisimamie uuzaji wa mazao ya chakula kiholela ili kuhifadhi chakula cha akiba